THIS IS SCAM ALERT >>

MATAPELI MAENEO YA SINZA DAR ES SALAAM ~ Nigerian 419 Scams

Wednesday 13 January 2016

MATAPELI MAENEO YA SINZA DAR ES SALAAM

Kuna hiki kisa nimetumiwa kutoka kwa mdau wangu.

Leo nimeitwa sinza palestina na mtu mwenye namba +255674860978 ili nimuuzie macbook pro for 1.2m. Kufika akanipigia simu niwasiliane na mdogo wake mwenye namba +255675355699 ili nimwoneshe mzigo maana ye hatokuwepo.

Nimefika sinza huyo mdogo wake akanipigia simu nikameet nae akanipeleka kwa mguu mpaka mahali anapodai ndo nyumbani kwa huyo bro wake anaeishi na mke wake.

Kuingia tukakaa nje nikamtolea mac akaikagua then alipoona ipo okay akasema nimsubiri akamwonyeshe huyo mke wa kaka yake ndo mwenye hela. Eti aichukue laptop sisi tusubiri kwa mbele yeye aende mlango wa nyuma anapodai ndo mke wa kaka ake anapokaa.

Kwa vile naufahamu utapeli wa njia hii nikamzuia asiondoke na hio mac amwite huyo shemeji yake aje aione wote tukiwepo.
Alipoona tumeshtukia akatuachia macbook kwamba tumsubiri akamwite.
TUUUUMEESUBIIIRIIIII (LOL).

kumbe karuka ukuta katokomea na hio sehemu wala hakuwa anaishi na yoyote aliyemfahamu. Tunampigia yule bro wa kwanza akanijibu "bahati yenu" akakata simu... Assholes!!

TAHADHARINI KUWENI MAKINI

Hawa watu wamejaa sana hapa dar please naombeni yoyote atakayepatwa na tukio la kitapeli ashare na sisi ili tujue ways tofauti ambazo wanazitumia ikiwezekana mpige na picha bila yeye kujua.

NAMBA NYINGINE ZA MATAPELI

+255675355699 anaitwa Martin tapeli maarufu sana pale sinza sokacity keshaliza watu kibao alafu hata hakimbii hilo eneo hata ukienda saivi unamkuta anajiamini sana sjui vipi.

Namba +255675355699 ni ya kakaake na Martin same scam methods as the one above) Below is the picture i took without him knowing while he was inspecting the macbook.

TUSHIRIKIANE KUTOKOMEZA UTAPELI... INAWEZEKANA!

0 comments:

Post a Comment

Please Tell Us What Do You Think About This Post!

.

.